MBINU 5 ZA KUANDAA KICHWA CHA MAKALA

kutokana na watanzania wengi kujiingiza katika hii industry ya blogging na website, na kwa harakaharaka watanzania wengi ni wamiliki wa website na blog na kuchangia upatikanaji wa habari na upatikanaji wa elimu kupitia makala ambazo wanaandaa na kuweka katika blog zao. Changamoto inatokea pale ambapo wanaitaji kuaandaa kichwa cha makala yake ambacho kitaongeza idadi ya watu na kupatikana katika search engine kama google,yahoo,bing na zingine.
Leo nakuletea makala hii nzuri ambayo iatjibu maswali yako na kukufanikisha malengo uliojiwekea katika blogging.


Tutaangalia sifa za kicha cha makala kizuri ambacho kinaongeza idadi ya watembeleaji katika website yako na blog yako kuinua kipato chako:-
  • kinatakiwa kiwe na mvuto kinchovutia watu kuingia na kusoma content.
  • kiwe na ukweli na yaliopo, sio kichwa cha makala na yaliopo ni tofauti kinawakasilisha. wasomaji na hawawezi kukuamini na kurudi tena kwenye website yako.
  • Kiwe ni rahisi kusomeka, epukana na font style,fontsize ambazo hazionekani,rangi ambazo hazionekani, kichwa cha habari ambacho hakisomeki watu hukipita 
  • Kichwa cha makala yako chatakiwa kuwa hai, hasa kama untumia verbs fanya kiwe hai mfano"7 Ways to be a Millionaire" kifanye kiwe"7 Ways to Generate Millions of Dollars"
  •  Kichwa kiwe kifupi, kichwa kirefu kinawafanya watu kuchoka na kuona uvivu kukisoma.
  • Kichwa cha makala chatakiwa kiwe halisi, kiwe kinahusiana moja kwa moja na maudhui ya makala yako ili kujenga uaminifu

NJIA TANO ZA KUANDIKA KICHWA CHA MAKALA KIZURI NA KINACHOONGEZA WATEMBELEAJI

  • Tumia herufi 

Hii ndo sababu waandishi wengi wa makala hutumia number kwenye vichwa vyao vya makala hasa magazeti, na mara nyingi hutumia number kuanzia 1 hadi 3 zinatumika vizuri mfano 17 na 19 zinatumika sana . Jaribu kufanya utafiti wa kuangalia magazeti mbalimbali ya mtandaoni
  • Tumia maneno yanayovuta umakini 

Tumia maneno yanyovutia na kuvuta umakini katika makala yako, mfano bure,muhimu,fun,absolute,strange,Incredible,Pain stacking, na mengine mengi yanayovuta umakini
  • Kiwe cha upekee  

Kama unaitaji kuorodhesha mambo fulani katika makala zako tumia maneno haya sababu,njia,siri,mbinu,idea,ukweli,sheria,
  • Tumia viulizi

Tumia maneno haya kama kwanini,kivipi,lini kwa kiingereza ni what,why,when,how ili kuleta utayali wa mtu kusoma makala yako ili iweze kujibu maswali yake aliyokuwa anajiuliza kila siku
  • Muahaidi msomaji

Weka maneno ambayo yataonyesha ahadi fulani ambayo msomaji wako ataipata atakapofungua makal yako na kumsaidia kujibu maswali yake, mara nyingi bold

  



Labels:

Post a Comment

Medson

{facebook#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {twitter#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {google-plus#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {pinterest#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {youtube#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL} {instagram#YOUR_SOCIAL_PROFILE_URL}

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget